Longhorn Mwanga wa Kiswahili Grade 3 (Rationalised)

Description
Longhorn Mwanga wa Kiswahili Kitabu cha Mwanafunzi, Gredi ya 3Â kimeandikwa kwa ustadi na umahiri mkubwa, kwa kutumia lugha inayofaa kiwango cha mwanafunzi wa Gredi ya Tatu. Kitabu hiki kinatosheleza kikamilifu mahitaji ya Mtaala wa Kiumilisi na malengo ya elimu ya taifa, kikishughulikia wanafunzi wote, wakiwemo wale wenye mahitaji maalumu na wanaoishi katika mazingira mbalimbali.
Vipengele Muhimu vya Ujifunzaji:
-
Mtaala wa Kiumilisi:Â Kinatosheleza kikamilifu mahitaji ya Mtaala wa Kiumilisi na malengo ya elimu ya taifa la Kenya, kikiwapa wanafunzi fursa ya kujenga umilisi muhimu.
-
Uwezo wa Mawasiliano:Â Kumwezesha mwanafunzi kuwa na uwezo wa kuwasiliana na kushirikiana kwa ufanisi na wenzake, na kukuza uadilifu na kujithamini.
-
Ujuzi wa Kidijitali:Â Kumwezesha mwanafunzi kutumia vifaa mbalimbali vya kidijitali na kuchanganua msimbo wa QR ili kupata matini za kidijitali, video na sauti.
-
Ushirikiano wa Mzazi:Â Kumshirikisha mzazi au mlezi kwa kina katika shughuli za ziada kwa njia rahisi ya kuelimisha na kuburudisha.
-
Marudio ya Kuchangamsha:Â Kuwapa wanafunzi mazoezi ya marudio mwishoni mwa kila suala kuu ili kuwachangamsha na kuwafanya wakumbuke kwa urahisi yale waliyojifunza.
Kitabu hiki kina mwongozo wa mwalimu na majibu tarajiwa kwa mazoezi yote, na ni nyenzo bora ya kukuza Kiswahili angavu miongoni mwa wanafunzi.
ISBN:Â 9789966644947












