Storymoja Smart Beginners Cheche Kiswahili GD3 (Rationalised)

Description
Storymoja Smart Beginners Cheche za Kiswahili Kitabu Cha Mwanafunzi Gredi ya 3Â kimeandikwa kwa kuzingatia yaliyomo kwenye ruwaza ya Mtaala wa Kiumilisi (CBC) ili kumfaa mwanafunzi kutekeleza shughuli mbalimbali za ujifunzaji. Shughuli zilizopendekezwa katika kitabu hiki zitamwezesha mwanafunzi kuwa na umilisi wa stadi mbalimbali za lugha ya Kiswahili.
Vipengele Muhimu:
-
Mtaala Mpya:Â Inashughulikia vipengele vyote vya mada mbalimbali kwa mujibu wa mtaala mpya wa Kiumilisi.
-
Picha na Michoro Angavu:Â Picha na michoro angavu kwa ajili ya kumwezesha mwanafunzi kuelewa matini na dhana za kiswahili.
-
Shughuli Tagusani:Â Shughuli tagusani kuhusu mada mbalimbali kwa mujibu wa ruwaza ya mtaala mpya.
-
Uhusishaji wa TEHAMA:Â Ujumuishaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika shughuli za ufunzaji na ujifunzaji wa Kiswahili.
-
Ushirikishaji na Maswala Mtambuko:Â Ushirikishaji wa wanafunzi wenye mahitaji maalum na ujumuishaji wa maswala mtambuko katika shughuli za ujifunzaji.
Kitabu hiki kimeandikwa na walimu wenye tajriba pana na kimeandamana na Mwongozo wa Mwalimu wenye maelezo ya kina.
ISBN:Â 9789914467017













